Ticker

6/recent/ticker-posts

Tabia Azindua Kampeni Mbili Kwa Vijana



Waziri wa Habari, Vijana  Vijana, Utamaduni na Michezo, Tabia Maulid Mwita  amewataka vijana  kuzitumia fursa zinazotolewa na Baraza la Vijana Zanzibar kwa lengo la kutatua changamoto mabalimbali  zinazowakabili.

Akizindua kampeni ya Program ya Mobile Youth Space (MYS) na Kampeni ya ’’Amani ni Tunu, Vijana Tuitunzeni’’, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana, tamaduni na Michezo, kwa naiba ya Wizara hiyo Mh Tabia Maulid Mwita amesema vijana bado wanakabiliwa na changamoto ya ushiriki na ushirikishwaji hususan katika mambo yanayowahusu na hatimae kukosa fursa na nafasi mbalimbali katika jamii ikiwemo ajira na uongozi katika ngazi za maamuzi.

Amesema Sera ya Maendeleo ya vijana ya Zanzibar ya 2013, imeonesha wazi changamoto ya ushiriki na ushirikishwaji wa vijana katika ngazi za maamuzi, kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo ya Kitaifa katika Nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa licha ya jitihada mbalimbali zinazochukuliwa.

“ Ushiriki wenye tija kwa vijana ni nguzo sahihi ya upatikanaji wa taarifa zinzowahusu na hatimae kuleta tija iliokusudiwa’’, Waziri Tabia.

Amesema Programa hiyo itatekelezwa kupitia mikutano ya wazi (Public meeting) inalenga kuwafikia vijana 39,600 katika Wilaya zote za Unguja na Pemba na kujumuisha shughuli mbali mbaliza utoaji elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii na vipeperushi.



Mapema Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar, Ali Haji  amesema vijana wana nafasi kubwa ya kulinda tunu ya Amani na utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025, kuijiunga katika mabaraza ya vijana bila kujali itikadi ya vyama kwa lengo la kunufaika na fursa zinazotolewa na pamoja na kulinda Amani ya nchi.

“Mabaraza ya vijana ni yenu, naomba muyatumie ili kueleza changamoto zenu na kujiletea maendeleo”, Ali Haji, Katibu Mtendaji, Baraza la Vijana Zanzibar.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi  kutoka Kijij cha kulelea watoto yatima Zanzibar (SOS )Gharib Abdalla Hamad amesema shirika hilo ni wadau wakubwa wa maendeleo ya vijana hivyo wataendelea kuunga mkono juhudi za wizara hiyo ili kuweza kufikiwa kwa maendeleo bora ya vijana hapa nchini.

Program ya MYS inatarajiwa kutekelezwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, kupitia Baraza la Vijana kwa kushirikiana na Shirika la SOS kwa kipindi cha miaka 3, kutoka April 2025 hadi April 2028, iliobeba ujumbe ’’ USHIRIKI NA USHIRIKISHWASJI NA UPATIKANAJI WA TAARIFA SAHIHI KWA VIJANA NI MSINGI WA MAENDELEO ENDELEVU’’.

 

Post a Comment

0 Comments