Ticker

6/recent/ticker-posts

Miongozo Na Sera Za Watu Wenye Ulemvau Haitoshelezi

 


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Abeida Rashid Abdallah amesema Miongozo na Sera inayohusu Watu Wenye Ulemavu kwa sasa haitosherelezi hivyo ipo haja ya kuangalia Sera na Sheria zingine namna ilivyowajumuisha Watu Wenye Ulemavu ili kuhakikisha kwamba hakuna kundi ambalo limeachwa nyuma katika jamiii.

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akifungua mkutano wa programu ya Kimataifa ya Haki za Watu Wenye Ulemavu, uliyofanyika katika ukumbi wa Goden Tulip, Uwanja wa Ndege, Unguja.

Amesema Sera ya mwaka 2004 inayohusu Watu Wenye Ulemavu haitosherelezi hivyo ipo haja ya kuangalia Sera na sheria zingine namna ilivyowajumuisha Watu Wenye Ulemavu. Alieza kama hakuna basi Watu Wenye Ulemavu wanalazimika kupaza sauti zao kwa kuwaambia jamii changamoto zinazowakabili  kutokana na mapungufu yaliyopo kwenya Sera na Sheria iliyopo.

"Miongozo na Sera ya 2004 ambayo inawajumuisha Watu Wenye Ulemavu ipo ambapo   kupitia programu hii ya kikao cha leo inafanyiwa review hivyo lazima tushukuru. Lakini pale ambayo tunaona mapungufu lazima tuwaoneshe wenzetu nini tunahitaji” Alisema bi Abeida.

Aidha bi Abeida amesema muda sio mrefu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto itazindua  Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kumpambana na vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambapo Mpango huo umezingatia masuala ya Watu Wenye Ulemavu.

Pia alitoa wito kwa Watu Wenye Ulemavu kuweka takwimu zao ingawa Serikali inaweka lakini ni vyema na wao wenyewe kuweka takwimu zao vizuri ili ziweze kuwasaidia wakati wa kutoa maoni yao.

Mwisho Bi Abeida amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suhuhu Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinnyi kwa uongozi wao pamoja na kuzingatia masuala ya Usawa wa Kijinsia na masuala ya Watu Wenye Ulemavu.

Mapema akizungumza Mtaalamu wa Ushauri masuala ya Usawa wa Kijinsia bi Maja Hansen Amesema mkutano huo wa Haki za Watu Wenye Ulemavu umelenga kuzungmzia ajenda nne ikiwemo Ushiriki na Ushirikishaji, Ulinzi wa vitendo vya ukatili kwa  Watu Wenye Ulemavu, Maboresho ya Sera, na Masuala ya takwimu  ambapo anaamini mkutao huo utaleta tija.

Kwa upande wa washiriki wa Mkutano huo, akizungumza Ali Omar Makame kutoka Shirikisho la Jumuiya la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA) amesema amefurahishwa na hatua ya waandaji wa mkutano huo walivyowashirikisha Watu Wenye Ulemavu katika kikao hicho, kwani wataweza kueleza  changamoto zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa vyoo  rafiki kwa baadhi ya majengo ya Serikali na Binafsi.

 

 

Post a Comment

0 Comments