Ticker

6/recent/ticker-posts

Simba, Yanga Kukutana Oktoba 19

 


Bodi ya ligi Tanzania bara imetua ratiba ya ligi kuu soka Tanzania Bara ambapo miamba ya soka Tanzania Simba Na Yanga imepangwa kukutana Oktobar 19, 2024 katika Dimba la KMC majira ya Saa 11: za jioni.

Miamba hiyo itakuwa ni mara ya pili kukutana kwa msimu huu ambapo mara ya kwanzi ilikutana Agosti 08, 2024 kwenye mchezo wa ngao ya jamii na Yanga kupata ushindi wa 1-0 lililopachikwa kimiani na Kiungo mshambuliaji Max Nzingeli mnamo dakika ya 44.

Kwenye ligi kuu msimo uliopita Yanga ilipata ushindi katika michezo yote miwili ambapo mchezo wa awali walishinda 5-1 huku mchezo wa pili ikipata ushindi wa 2-1.

Post a Comment

0 Comments