Ticker

6/recent/ticker-posts

Dkt. Mwinyi Ashiriki Maziko Ya Mama Mzazi Wa Mwenyekiti Wa ZAVA

 


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi,Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi Leo Jumamosi Julai 20, 2024 amejumuika pamoja na Viongozi Wakuu, Masheikh, na Waumini mbali mbali wa Kiislamu, katika Maziko ya Bi. Zuleikha bint Ahmad ambaye ni mama Mzazi wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Zanzibar (ZAVA) Kassim Haidar.

Marehemu amesaliwa Msikiti wa Ijumaa Malindi,  ambapo Sala imeongozwa na Mtoto wake, Sheikh Ahmad Haidar na kuzikwa katika Makaburi ya hapo hapo Msikitini, Mkoa wa Mjini-Magharibi, Unguja.

Viongozi wengine wa Serikali, Dini na Jamii wamehudhuria Maziko hayo ikiwa ni pamoja na Makamu wa kwanza Wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhaj Othman Massoud Othman, Makamu wa Pili wa Rais Alhaj Hemed Suleiman Abdulla, Spika wa baraza la Wawakilishi Zanzibar Zubeir Ali Maulid na Mufti mkuu wa Zanzibar Saleh Omar Kabi.

Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi, Amiin!

Innalillahi Waina Ilayhi Raajiun!

Post a Comment

0 Comments